17 Apr 2024 / 70 views
Pochettino akasirishwa na wachezaji wake

Kocha wa Chelsea, Mauricio Pochettino amesema kuwa alikasirishwa na mzozo wa nani angepiga penalti katika ushindi wao wa 6-0 dhidi ya Everton na amewaonya wachezaji wake kutorudia tena.

Nicolas Jackson na Noni Madueke walibishana kuhusu nani angepiga mkwaju wa penalti, kabla ya Cole Palmer mfungaji wa kawaida wa Chelsea kufunga bao lake la nne.

"Siwezi kukubali aina hii ya tabia," alisema Pochettino. "Niliwaambia ni mara ya mwisho nataka kuona tabia ya aina hii."

Aliongeza: "Haiwezekani kuwa na aina hii ya tabia baada ya utendaji huu. Ikiwa tunataka kuwa timu kubwa, tunahitaji kubadilika na kufikiri kwa pamoja."

Palmer alifunga penalti ya dakika ya 64 kwa The Blues mkwaju wake wa tisa wa penalti uliofaulu msimu huu kufuatia pambano lisilo la kawaida la sekunde 60 lililohusisha wachezaji watano.

Thiago Silva kisha akaingilia kati, huku Jackson akiondoka. Nahodha Conor Gallagher kisha akamsogelea Madueke, akimnyooshea kidole Palmer na kumwambia akabidhi mpira.

Madueke aliwakataa watu wote wawili, kabla ya Gallagher kunyakua mpira na kumpa Palmer.

Palmer na kisha Gallagher walilazimika kumfukuza Jackson, ambaye alirudi kujihusisha tena, kisha msukumo wa mwisho kutoka kwa Gallagher kwenye Madueke ukamaliza ugomvi.